Chris Brown ataja jina la mtoto wake kwa style hii
CHRIS Brown ametuonesha jina la mtoto wake wa pili ambaye alitajwa kuzaliwa November 20 mwaka huu na mrembo Ammika Harris.
Kama ambavyo alitutambulisha kuzaliwa kwa mtoto huyo wa Kiume, Breezy ametutajia na jina kwa staili hiyo hiyo. Kwenye post yake ya masaa machache hapa instagram akiwa amevaa Jaketi lililoandikwa “Roro & Aeko” upande wa kushoto.
Hii imetafsiriwa kwamba; “Roro” ni jina la utani la binti yake Royalty, na “Aeko” linaweza kuwa jina la mtoto wake huyo wa Kiume. Kwenye caption ambayo tayari ameifuta aliandika; RORO & AEKO (ECHO)
Naona hii ndio namna ambayo Chris Brown anatumia kumtambulisha mtoto wake huyu wa Pili, alivaa Sweta lililoandikwa “BORN” siku (Nov. 20) ambayo inatajwa mwanadada Ammika Harris alijifungua.
Toa Maoni Yako Hapa