The Weekend Akiri Kukasirishwa na Wimbo wa Usher Raymond
Mkali wa masauti The Weekend ambaye kwa sasa anatamba na album yake ‘After Hours’ amezungumzia namna alivyopokea wimbo wa Usher Raymond uitwao ‘Climax’ ambao ulitoka mwaka 2012.
Msanii huyo anasema kwamba alipousikia wimbo huo alishangaa na kukasirika kwa wakati mmoja. “Niliusikia wimbo wa Usher, nikasema hapana huu ni wimbo wangu” najua nilikuwa nafanya jambo sahihi ila nilikasirika kusikia unasikika kama mimi ndiye niliyeimba.
Wawili hao hawajawahi kufanya kazi pamoja. Mwaka 2016 The Weekend aliomba msamaha hadharani kwa kusema kuwa Usher Raymond ndiye msanii mwenye tuzo nyingi za Billboard za usiku mmoja akimaanisha bila kufanya juhudi kubwa.
Toa Maoni Yako Hapa