Ariana Grande, Mwanamke Wa Kwanza Kufikisha Wafuatiliaji Milioni 200 Instagram
Msanii, Ariana Grande, ameungana na Christiano Ronaldo na kuwa miongoni mwa watu wenye wafuatiliaji zaidi ya milioni 200 kwenye kurasa zao za Instagram.
Mpaka sasa Ariana ana wafuasi 201M akifuatiwa na Kylie Jenner mwenye wafuasi milioni 194 na Selena Gomez mwenye wafuasi milioni 192.
Mtu wa kwanza kufikisha wafuatiliaji zaidi ya milioni 200 kwenye ukurasa wa Instagram ni Christiano Ronaldo ambaye mpaka sasa ana wafuasi milioni 237.
Toa Maoni Yako Hapa