MUME WA SHILOLE AWAJIBU WANAOMPONDA MKEWE
Mume wa msanii Shilole, Rommy 3D ameonyesha kutofurahishwa na wanaoponda muonekano wa unene wa mke wake huyo, na kuvunja ukimya kwa wote wanaotaka apungue kuwa hawaitakii mema ndoa yao. Haya yanakuja kufuatia mashabiki wa shilole kuuzungumzi muonekano wake .
“Wote wanaotaka mke wangu apungue hawaitakii mema ndoa yetu (ni wachawi) kwa sababu kwenye historia yangu sijawahi kupenda mwanamke kimbaumbau, napenda mabonge haswaaaa, wanaonijua wanajua,” alisema Rommy 3D.
Toa Maoni Yako Hapa